Mimi naitwa Isaack ni kijana mwenye miaka 28, nimeoa. Nimekuwa na mazoea ya kupiga punyeto kuanzia mwaka 2007 nikiwa mwaka wa kwanza chuo kikuu baada ya kuanza kuangalia picha za ngono. Licha ya kwamba nimeoa lakini naona kama siwezi kuacha mchezo huu. Nimekuwa nikisikia watu wakisema vijiweni kuwa mtu anayefanya masterbation anaweza kupoteza nguvu za kiume au kushindwa kumridhisha mke. Nikisikia stori hizo huwa naingiwa na hofu. Kwa sasa sina tatizo lolote na shemeji yenu anapata haki yake kama kawaida. Je nini madhara ya punyeto kama nitaendelea kwa muda mrefu?
Ni mimi
Isaack.
Clinic Yetu tayari imefunguliwa na ndugu yetu Isaack anakuwa wa kwanza kufungua mlango. Isaack anapenda kujua madhara ya punyeto. Hiyo ndo shida iliyomleta kwenye clinic...Msaidie Isaack....
ReplyDeleteMimi naona punyeto ni salama na aina madhara yoyote kiafya kwanza inaweza kukuepusha na maambukizi ya ugonjwa wa zinaa. Lakini kama uko kwenye ndoa hunasababu ya kufanya hivyo
ReplyDeleteTafiti zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimi 80 ya wanafunzi wa vyuo vikuu wamefanya mara moja ktk maisha yao....
ReplyDeleteNahitimisha mada hii kwa kumueleza bwana isaack kuwa punyeto haina madhara makubwa ingawaje mara chache huweza kusababisha uume kivunjika
ReplyDeletekama ulikuwa na makovu.Vingenevyo punyeto ni salama