Nami najitokeza kwa mara ya kwanza ktk huu ukurasa. Mimi naitwa James, mke wangu anamimba ya miezi miwili na ni mimba yetu ya kwanza. Amekuwa akisumbuliwa na kichefuchefu na mara nyingine anatapika. Nami nimepata matatizo kama hayo kwani siku za karibuni nimekuwa mchovu, na napata kichefuchefu. Nimekwenda hospitali nikafanywa vipimo sikuwa na ugonjwa wowote, lakini rafiki yangu kaniambia eti kwa sababu mke wangu ana mimba dalili zile zimeamia kwangu. Je ni kweli kwamba hiyo inaweza kutokea??
No comments:
Post a Comment